>
1. Samsung Galaxy S 2
|
Samsung Galaxy SII |
Kinachoifanya simu hii kuwa kileleni kwenye chati ni ubora wa vianisho halisi vyake, ina kasi na nguvu na pia ni simu nyebamba kuliko zote Duniani ambapo imeipiku iPhone 4 katika sifa hii. Ina kamera nzuri, yenye kutoa picha safi mno na uwezo wa kurekodi video za HD, vifuatavyo ni vianisho halisi vyake:-
Video: Full HD 1080p na megapiksel, ukiwa na simu hii basi huhitaji kamkoda wala kamera, simu nyingi kamera zake ni maskhara tu, lakini Galaxy S2 si hivyo ni kamera ya kweli yenye uwezo wa hali ya juu. Bila ya kutia chumvi unaweza hata kurekodi harusi iwapo utapata mwangaza wa kutosha.
Prosesa: Dual Core 1.2 Ghz aina ya snapdragon, hii ni prosesa yenye nguvu za kuendesha hata laptop wacha kijisimu, ina kasi kiasi kupindukia kasi inayohitajika kwenye simu.
Skrini: 4.3 Super Amoled Plus, hii inaifanya simu hii kuwa na skrini inayon’gara sana. Unaweza kutazama kwa pembe (angle) ya chini kabisa na kuona kwa vizuri na bila ya matatizo.
Kamera: megapiksel nane yenye flashi inaifanya simu hii kuwa na kamera yenye ufanisi kuliko zote kwenye simu, zipo simu zinazofanana na simu hii kwenye piksel hizi lakini mpaka sasa hakuna zaidi yake.
Umbile: Ikiwa na wembamba wa milimita 8.49 inaifanya simu hii kuwa ni simu nyembamba kuliko zote Duniani. Vile vile simu hii ina uwezo wa kutuma ujumbe mfupi kwa sauti ikitumia teknolojia ya Google ya kutambua sauti (voice recognition) na pia inatumia Android Gingerbread 2.3 ambayo ni toleo jipya la OS ya Android kwenye simu.
Simu hii imekamata kilele katika chati ya simu mwezi huu kwa kuipiku iPhone 4, je simu hii itaweza kubaki kileleni itakapotolewa iPhone 5 baina ya mwezi wa Juni na Septemba mwaka huu? Hatuna jibu, ni vyema tu tusubiri.
2. iPhone 4
|
iPhone 4 nyeupe |
Simu hii imekuwa kilele kwa muda wa zaidi ya miezi kumi, kutokana na wingi wa simu na namna simu zinavyobadilika haraka si rahisi kwa simu kuwa kwenye chati kwa zaidi ya mwezi mmoja, hii inathibitisha namna ambavyo simu hii ilizitangulia simu nyingine kwa wakati ilipotolewa. Yavutayo ndio yanaifhanya simu huu kuwa ni miongoni mwa si bora:
OS: iOS 4.3.3 yenye ubora, ikitumia OS ambayo haipatikani kwenye simu yoyote nyingine, inaifanya iPhone kukosa ushindani wa karibu kwenye nukta hii. OS hii ni rahisi kuitumia na ina ufanisi bora.
Appstore: Hili ni duka la kununulia apps (program), lina apps zaidi ya laki mbili, ni kweli kabisa kama Apple wanavyodai kwenye tangazo la simu hii “kama huna iPhone basi huna iPhone” Karibu kila unachofikiria ambacho ungependa simu yako ifanye basi kuna app yake kwenye duka hili.
Skrini: Skrini yake ambayo inaitwa Retina inaukubwa wa inchi 3.5 na piksel kwa kila inchi (ppi) ni 320. Uwezo wa jicho kuona ni mwisho ppi 300 unapikamata kitu kiasi cha umbali wa sentimita 25 hivi. Hii maana yake ni kwamba macho yetu hayana uwezo wa kuona uzuri wa skrini ya iphone, yaani ni nzuri kuliko tunavyoiona.
SSD: Huhitaji kukunua SD kadi kwani haitumii teknolojia hiyo. Hata hivyo ina disk aina ya SSD (solid State Disk) yenye ukubwa baina ya 16GB na 32GB. Apple wanadai kwamba kadi za SD hupnguza kasi za simu.
iTunes: Mawasiliano baina ya simu hii na kompyuta hufanywa kwa kutumia program ya iTunes, hii hurahisisha kazi ya ku-backup simu na kuingiza mafaili kama vile muziki, vitabu (E Books), picha, video na apps na pia kuhamisha video, picha na apps zilizo kwenye i`phone kwenda kwenye kompyuta kwa ajili ya kutumia au kuhifadhi.
Umbile: Simu hii ina umbile la kipekee, ambapo ina kioo mbele na nyumba, ni ya pili kwa wembamba baada ya Samsung Galaxy S2 ambapo ina wembamba wa milimita 9.3 na ina kona za kiduara zinazoifanya kukamatika kuwe ni rahisi .
3. HTC Sensation
|
HTC Sensation |
Huwezi kuzungumzia simu bora bila ya kuitaja HTC. Sensation kama jina lake ni simu ambayo ina ufanisi usiojificha.
Kuzima mlio: Simu hii kama zilivyo baadhi ya HTC, inapoita na ukaichukua na kuifunika kwa kuigeuza skrini kuelekea chini basi hunyamaza, ukiwa mkutanoni au darasani na umesahau kuitoa sauti basi hii teknolojia itakufaa sana wakati huo.
Vianisho halisi: Simu hii inafanana mambo mengi na Galaxy 2 ikiwa ni pamoja na Android Gingerbread , kamera yenye megapiksel nane, prosesa aina ya dula core yenye kasi ya 1.2 Ghz na ndio maana ipo karibu na juu kwenye chati hii.
Skrini: Ikiwa na ukubwa wa inchi 4.3 yenye mn’garo ulikithiri, uzuri skrini hii haitofautiani sana na skrini ya Samsung Galaxy S2.
HTC Sense: simu hii pia imevalishwa koti ya HTC Sense ambapo linaweza kukufanya usahau kama unatumia Android kwa namna koti hili lilivyo la kipekee. HTC Sense inaonyesha habari muhimu kwa urahisi ikiwa ni pamoja na hali ya hewa, saa na tarehe katika mji uliopo, unaposafiri basi HTC Sense kwa kutumia sensa za GPS nayo hubadilika wenyewe kwa mujibu wa mji uliopo
HTC Sync: HTC sensation pia hutumia HTC Sync kuhamisha mafaili baina yake na kompyuta na hivyo kuifanya kazi hii kuwa ni rahisi kwa kiasi fulani tofauti na chukua na weka (drg and drop) inayotumika kwenye simu nyingine.
Umbile: Simu hii pia ina upana wa milimita 11 pana kwa milimita 2 tu ukifanannisha na iPhone bado inapendeza kwa kuiona na kuishika mkononi ni rahisi. Pia gamba lake limetengeneswa kwa namna ambayo HTC wenye we wanaiita ‘unibody’ yaani halina kufungwa msumari wala kuunganishwa unganishwa.
4. Motorola Atrix Laptop
|
Motorola Atrix |
Simu hii ni moto kama ulivyo uhamasishaji wa Motorola ‘Moto’. Motorola wanastahiki kupengezwa kwa uvumbuzi wa kisasa walioufanya kwenye Atrix.
Dock: Doki hii hujulikana kama HD multimedia dock. Hichi kifaa ambacho unaiweka simu hii hukuwezesha kutumia internet ya simu kwenye kompyuta yako. Doki hii inakuwezesha kuunganisha simu hii na TV, kompyuta, skrini, mouse na keyboard kwa kutumia USB na HDMI.
Lapdock: Pia Atrix ina kifaa kijulikanacho kama Lapdock. Hii huigeuza Atrix kuwa laptop kamili. kila kilichomo kwenye simu inapokwa simu hii kwenye lapdock huwa kinaweza kupatikana kwenye lapdock ikiwa ni pamoja na mtandao wa simu, mafaili ya picha, muziki au video yaliyopo kwenye simu. Pia lapdock hii inauwezo ya kuonesha HD.
|
Lapdock na Atrix ikiwa imepachikwa |
Vianisho halisi: Simu hii pia ni Android ambayo ilipotoka ilitumia toleo la Froyo 2.2 lakini kwa sasa unaweza kuiboresha na kuweka Android 2.3 Gingerbread. ina kamera yenye megapiksel 5.
Fingerprint: Simu hii ina usalama mkubwa. Ina teknolojia ya fingerprint inayokuwezesha kuitia loki na hivyo ni aliyeifunga tu kwa kutumia vidole ndiye utakaeweza kuifungua. Huna haja ya kukumbuka neno lasiri (password) wala kuwa na wasi wasi wa mtu wa karibu yako kuweza kujua neno la siri unalotumia
Hivyo badala ya kununua laptop na Simu waweza kununua Motorola Atrix na lapdock yake, ikiwa unataka kutumia kwa ajili ya kujifurahisha kwa video, muziki na picha basi dock maalum kwa shughuli hii (entertainment dock) hakitkufanya ujihisi kwamba umepungukiwa.
Sehemu ya pili ya makala hii tutazielezea simu zenye kushika nafasi ya sita hadi ya kumi nazo ni:
Sony Ericsson Xperia Arc
Google Nexus S
LG Optimus 2X
HTC Desire S
HTC Incredible S
Samsung Galaxy S